27. Mtu mwovu hupanga uovu;maneno yake ni kama moto mkali.
28. Mtu mpotovu hueneza ugomvi,mfitini hutenganisha marafiki.
29. Mtu mkatili humshawishi jirani yake;humwongoza katika njia mbaya.
30. Anayekonyeza jicho kwa hila amepanga maovu;anayekaza midomo amekwisha nuia mabaya.
31. Kuwa na mvi za uzee ni taji la utukufu;hupatikana kwa maisha ya uadilifu.
32. Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwenye nguvu;aitawalaye nafsi yake ni bora kuliko autekaye mji.
33. Kura hupigwa kujua yatakayotukia,lakini uamuzi ni wake Mwenyezi-Mungu.