Methali 16:19-23 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Afadhali kuwa mnyenyekevu na kuwa maskini,kuliko kugawana nyara na wenye kiburi.

20. Anayezingatia mafundisho atafanikiwa;heri mtu yule anayemtumainia Mwenyezi-Mungu.

21. Mwenye hekima moyoni huitwa mwenye akili;neno la kupendeza huwavutia watu.

22. Hekima ni chemchemi ya uhai kwake aliye nayo,bali upumbavu ni adhabu ya wapumbavu.

23. Moyo wa mwenye hekima humwezesha kusema kwa busara;huyafanya maneno yake yawe ya kuvutia.

Methali 16