Methali 16:11-18 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenyezi-Mungu hutaka kipimo na mizani halali;mawe yote mfukoni ya kupimia ni kazi yake.

12. Ni chukizo kubwa wafalme kutenda uovu,maana msingi wa mamlaka yao ni haki.

13. Mfalme hupendelea mtu asemaye kwa unyofu;humpenda mtu asemaye ukweli.

14. Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo;mtu mwenye busara ataituliza.

15. Uso wa mfalme ukingaa kuna uhai;wema wake ni kama wingu la masika.

16. Kupata hekima ni bora kuliko dhahabu;kupata akili ni chaguo bora kuliko fedha.

17. Njia ya wanyofu huepukana na uovu;anayechunga njia yake huhifadhi maisha yake.

18. Kiburi hutangulia maangamizi;majivuno hutangulia maanguko.

Methali 16