Methali 15:7-12 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.

8. Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini sala ya wanyofu humfurahisha Mungu.

9. Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini Mungu huwapenda wale wafuatao mambo adili.

10. Adhabu kali ipo kwa wanaoacha mwenendo mwema;yeyote achukiaye kuonywa atakufa.

11. Ikiwa Mwenyezi-Mungu ajua yaliyo Kuzimu na Abadoni,mawazo ya binadamu yatawezaje kujificha mbele yake?

12. Mwenye madharau hapendi kuonywa,hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.

Methali 15