7. Mdomo wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
8. Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini sala ya wanyofu humfurahisha Mungu.
9. Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini Mungu huwapenda wale wafuatao mambo adili.
10. Adhabu kali ipo kwa wanaoacha mwenendo mwema;yeyote achukiaye kuonywa atakufa.
11. Ikiwa Mwenyezi-Mungu ajua yaliyo Kuzimu na Abadoni,mawazo ya binadamu yatawezaje kujificha mbele yake?
12. Mwenye madharau hapendi kuonywa,hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.