24. Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,ili aepe kuingia chini kuzimu.
25. Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.
26. Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,bali maneno mema humfurahisha.