Methali 15:22-27 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Mipango huharibika kwa kukosa shauri,lakini kwa washauri wengi, hufaulu.

23. Kutoa jibu sahihi hufurahisha;neno lifaalo kwa wakati wake ni jema mno!

24. Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,ili aepe kuingia chini kuzimu.

25. Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.

26. Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,bali maneno mema humfurahisha.

27. Anayetamani faida ya ulanguzianaitaabisha jamaa yake,lakini achukiaye hongo ataishi.

Methali 15