22. Mipango huharibika kwa kukosa shauri,lakini kwa washauri wengi, hufaulu.
23. Kutoa jibu sahihi hufurahisha;neno lifaalo kwa wakati wake ni jema mno!
24. Njia ya mwenye hekima huelekea juu kwenye uhai,ili aepe kuingia chini kuzimu.
25. Mwenyezi-Mungu huyabomoa makao ya wenye kiburi,lakini huilinda mipaka ya makao ya mjane.
26. Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,bali maneno mema humfurahisha.
27. Anayetamani faida ya ulanguzianaitaabisha jamaa yake,lakini achukiaye hongo ataishi.