Methali 14:9-12 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Wapumbavu huchekelea dhambi,bali wanyofu hupata fadhili kwa Mungu.

10. Moyo waujua uchungu wake wenyewe,wala mgeni hawezi kushiriki furaha yake.

11. Nyumba ya mtu mwovu itabomolewa,lakini hema ya wanyofu itaimarishwa.

12. Njia unayodhani kuwa ni sawa,mwishoni yaweza kukuongoza kwenye kifo.

Methali 14