Methali 14:31-35 Biblia Habari Njema (BHN)

31. Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake,lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.

32. Mwovu huangamizwa kwa matendo yake maovu,lakini mwadilifu hupata usalama kwa unyofu wake.

33. Hekima imo moyoni mwa mtu mwenye busara;haipatikani kamwe mioyoni mwa wapumbavu.

34. Uadilifu hukuza taifa,lakini dhambi ni balaa kwa taifa lolote.

35. Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima,lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Methali 14