29. Mtu asiye mwepesi wa hasira ana busara kubwa,lakini akasirikaye upesi hukuza upumbavu.
30. Amani rohoni humpa mtu afya,lakini tamaa huozesha mifupa.
31. Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake,lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.
32. Mwovu huangamizwa kwa matendo yake maovu,lakini mwadilifu hupata usalama kwa unyofu wake.
33. Hekima imo moyoni mwa mtu mwenye busara;haipatikani kamwe mioyoni mwa wapumbavu.
34. Uadilifu hukuza taifa,lakini dhambi ni balaa kwa taifa lolote.
35. Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima,lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.