26. Amchaye Mwenyezi-Mungu ana tumaini imara,na watoto wake watapata kimbilio salama.
27. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni chemchemi ya uhai;humwezesha mtu kuepa mitego ya kifo.
28. Fahari ya mfalme ni wingi wa watu wake,lakini bila watu mtawala huangamia.
29. Mtu asiye mwepesi wa hasira ana busara kubwa,lakini akasirikaye upesi hukuza upumbavu.
30. Amani rohoni humpa mtu afya,lakini tamaa huozesha mifupa.
31. Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake,lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.
32. Mwovu huangamizwa kwa matendo yake maovu,lakini mwadilifu hupata usalama kwa unyofu wake.