Methali 14:19-26 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Waovu watapiga magoti mbele ya watu wema,watu wabaya mlangoni mwa waadilifu.

20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake,lakini tajiri ana marafiki wengi.

21. Anayemdharau jirani yake ni mwenye dhambi,bali ana heri aliye mwema kwa maskini.

22. Anayepanga maovu kweli anakosea!Wanaopanga kutenda mema hufadhiliwa.

23. Bidii katika kila kazi huleta faida,lakini maneno matupu huleta umaskini.

24. Mali ni taji ya fahari ya wenye hekima,lakini ujinga ni shada la wapumbavu.

25. Shahidi wa kweli huokoa maisha,lakini msema uongo ni msaliti.

26. Amchaye Mwenyezi-Mungu ana tumaini imara,na watoto wake watapata kimbilio salama.

Methali 14