Methali 14:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,lakini mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

2. Mwenye mwenendo mnyofu humcha Mwenyezi-Mungu,lakini mpotovu humdharau Mungu.

3. Mpumbavu hujiadhibu mwenyewe kwa kuropoka kwake,lakini mwenye hekima hulindwa na maneno yake.

4. Bila ng'ombe wa kulima ghala za mtu ni tupu,mavuno mengi hupatikana kwa nguvu ya ng'ombe wa kulima.

5. Shahidi mwaminifu hasemi uongo,lakini asiyeaminika hububujika uongo.

Methali 14