Methali 13:8-12 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Fidia ya mtu ni mali yake,lakini maskini hana cha kutishwa.

9. Mwadilifu hungaa kama taa iwakayo vizuri,lakini waovu ni kama taa inayozimika.

10. Kiburi husababisha tu ugomvi,lakini kwa wanaokubali shauri jema mna hekima.

11. Mali ya harakaharaka hutoweka,lakini akusanyaye kidogokidogo ataiongeza.

12. Tumaini la kungojangoja huumiza moyo,lakini tazamio linalotimia ni mti wa uhai.

Methali 13