Methali 13:18-22 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Umaskini na fedheha humpata asiyejali mafundisho,lakini mwenye kusikia maonyo huheshimiwa.

19. Inafurahisha upatapo kile unachotaka,kwa hiyo wapumbavu huchukia kuepa uovu.

20. Anayeandamana na wenye hekima hupata hekima,lakini anayejiunga na wapumbavu atapata madhara.

21. Watendao dhambi huandamwa na balaa,lakini waadilifu watatuzwa mema.

22. Mtu mwema huwaachia urithi uzao wake,lakini mali ya mwenye dhambi imerundikiwa waadilifu.

Methali 13