11. Mali ya harakaharaka hutoweka,lakini akusanyaye kidogokidogo ataiongeza.
12. Tumaini la kungojangoja huumiza moyo,lakini tazamio linalotimia ni mti wa uhai.
13. Anayedharau mawaidha anajiletea maangamizi,lakini anayetii amri atapewa tuzo.
14. Mafundisho ya wenye hekima ni chemchemi ya uhai;humwezesha mtu kuiepa mitego ya kifo.
15. Kuwa na akili huleta fadhili,lakini njia ya waovu ni ya taabu
16. Mwenye busara hutenda kila kitu kwa akili,lakini mpumbavu hutembeza upumbavu wake.