Methali 11:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Anayetegemea mali zake ataanguka,lakini mwadilifu atastawi kama jani bichi.

29. Anayeivunja nyumba yake ataambua upepo.Mpumbavu atakuwa mtumwa wa wenye hekima.

30. Matendo ya mwadilifu huleta uhai,lakini uhalifu huuondoa uhai.

31. Ikiwa mwadilifu hupata tuzo hapa duniani,hakika mwovu na mwenye dhambi atapatilizwa.

Methali 11