3. Mwenyezi-Mungu hawaachi waadilifu wapate njaa,lakini huzipinga tamaa za waovu.
4. Uvivu husababisha umaskini,lakini mkono wa mtu wa bidii hutajirisha.
5. Mwenye busara hukusanya wakati wa mavuno,kulala wakati wa kuvuna ni aibu.
6. Mwadilifu hujiletea baraka yeye mwenyewe,lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na ukatili.