Methali 10:16-19 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Tuzo la mtu mwema ni uhai,lakini mwovu huishia katika dhambi.

17. Anayekubali maonyo anaelekea kwenye uhai,lakini anayekataa kuonywa amepotoka.

18. Amchukiaye mwingine kwa siri ni mnafiki,anayemsingizia mtu ni mpumbavu.

19. Penye maneno mengi hapakosekani makosa,lakini aneyeuzuia ulimi wake ana busara.

Methali 10