Methali 1:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.

7. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa maarifa,lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.

8. Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,wala usiyapuuze mafundisho ya mama yako;

9. hayo yatakupamba kilemba kichwani pako,kama mkufu shingoni mwako.

10. Mwanangu, usikubali kushawishiwa na wenye dhambi.

11. Wakisema: “Twende tukamvizie mtu na kumuua;njoo tukawashambulie wasio na hatia!

Methali 1