Methali 1:27-33 Biblia Habari Njema (BHN)

27. hofu itakapowakumba kama tufani,maafa yenu yatakapowavamia kama kimbunga,wakati udhia na dhiki vitakapowapata.

28. Hapo ndipo mtakaponiita lakini sitaitika;mtanitafuta kwa bidii lakini hamtanipata.

29. Kwa kuwa mliyachukia maarifa,wala hamkuchagua kumcha Mwenyezi-Mungu;

30. maadamu mlikataa shauri langu,mkayapuuza maonyo yangu yote;

31. basi, mtakula matunda ya mienendo yenu,mtavimbiwa kwa hila zenu wenyewe.

32. Maana wajinga hujiua kwa ukaidi wao,wapumbavu hujiangamiza kwa kujiamini kwao.

33. Lakini kila anisikilizaye atakaa salama,atatulia bila kuogopa mabaya.”

Methali 1