Mathayo 4:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Roho alimwongoza Yesu mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi.

2. Akafunga siku arubaini mchana na usiku, na mwishowe akaona njaa.

3. Basi, mshawishi akamjia, akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

4. Yesu akamjibu, “Imeandikwa:‘Mtu haishi kwa mkate tu,ila kwa kila neno asemalo Mungu.’”

5. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, mji mtakatifu, akamweka juu ya mnara wa hekalu,

Mathayo 4