Mathayo 27:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Naye akazitupa zile fedha hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.

6. Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya hekalu kwa maana ni fedha za damu.”

7. Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.

8. Ndio maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.

9. Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walichukua vipande thelathini vya fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walimtia bei,

Mathayo 27