Mathayo 25:6-18 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Usiku wa manane kukawa na kelele: ‘Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.’

7. Hapo wale wasichana wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.

8. Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: ‘Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.’

9. Lakini wale wenye busara wakawaambia, ‘Hayatatutosha sisi na nyinyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!’

10. Basi, wale wasichana wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wasichana waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la harusi, kisha mlango ukafungwa.

11. Baadaye wale wasichana wengine wakaja, wakaita: ‘Bwana, Bwana, tufungulie!’

12. Lakini yeye akawajibu, ‘Nawaambieni kweli, siwajui nyinyi.’”

13. Kisha Yesu akasema, “Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.

14. “Wakati huo itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ngambo: Aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.

15. Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: Mmoja fedha talanta tano, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.

16. Mara yule aliyekabidhiwa fedha talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.

17. Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.

18. Lakini yule aliyekabidhiwa fedha talanta moja akaenda, akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.

Mathayo 25