Mathayo 25:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Wakati huo, ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.

2. Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.

3. Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.

4. Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.

5. Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wasichana wote walisinzia, wakalala.

6. Usiku wa manane kukawa na kelele: ‘Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.’

7. Hapo wale wasichana wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.

8. Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: ‘Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.’

9. Lakini wale wenye busara wakawaambia, ‘Hayatatutosha sisi na nyinyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!’

Mathayo 25