Mathayo 22:37-45 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Yesu akamjibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote’.

38. Hii ndiyo amri kuu na ya kwanza.

39. Ya pili inafanana na hiyo: ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe’.

40. Sheria yote ya Mose na mafundisho ya manabii vinategemea amri hizi mbili.”

41. Mafarisayo walipokusanyika pamoja, Yesu aliwauliza,

42. “Nyinyi mwaonaje juu ya Kristo? Je, ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Wa Daudi.”

43. Yesu akawaambia, “Basi, inawezekanaje kwamba kwa nguvu ya Roho Mtakatifu Daudi anamwita yeye Bwana? Maana alisema:

44. ‘Bwana alimwambia Bwana wangu:Keti upande wangu wa kulia,mpaka niwaweke maadui zako chini ya miguu yako.’

45. Basi, ikiwa Daudi anamwita Kristo ‘Bwana,’ anawezaje kuwa mwanawe?”

Mathayo 22