35. Mmoja wao, mwanasheria, akamwuliza Yesu kwa kumjaribu,
36. “Mwalimu, ni amri ipi iliyo kuu katika sheria?”
37. Yesu akamjibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote’.
38. Hii ndiyo amri kuu na ya kwanza.
39. Ya pili inafanana na hiyo: ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe’.
40. Sheria yote ya Mose na mafundisho ya manabii vinategemea amri hizi mbili.”
41. Mafarisayo walipokusanyika pamoja, Yesu aliwauliza,