21. Wakamjibu, “Ni ya Kaisari.” Hapo Yesu akawaambia, “Basi, ya Kaisari mpeni Kaisari, na ya Mungu mpeni Mungu.”
22. Waliposikia hivyo wakashangaa; wakamwacha, wakaenda zao.
23. Siku hiyo, baadhi ya Masadukayo wasemao wafu hawafufuki walimwendea Yesu.
24. Basi, wakamwambia, “Mwalimu, Mose alisema mtu aliyeoa akifa bila kuacha watoto, lazima ndugu yake amwoe huyo mama mjane, ili ampatie ndugu yake watoto.
25. Basi, hapa petu palikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa kisha akafa bila kujaliwa watoto, akamwachia ndugu yake huyo mke wake mjane.
26. Ikawa vivyo hivyo kwa ndugu wa pili, na wa tatu, mpaka wa saba.
27. Baada ya ndugu hao wote kufa, akafa pia yule mama.
28. Je, siku wafu watakapofufuka mama huyo atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba? Maana wote saba walikuwa wamemwoa.”
29. Yesu akawajibu, “Nyinyi mmekosea kwa sababu hamjui Maandiko Matakatifu wala nguvu ya Mungu.
30. Maana wafu watakapofufuka hawataoa wala kuolewa; watakuwa kama malaika mbinguni.