1. Yesu alisema nao tena kwa kutumia mifano:
2. “Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme aliyemwandalia mwanawe karamu ya harusi.
3. Basi, akawatuma watumishi kuwaita walioalikwa waje harusini, lakini walioalikwa hawakutaka kufika.
4. Akawatuma tena watumishi wengine, akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa: Karamu yangu iko tayari sasa; fahali wangu na ndama wanono wamekwisha chinjwa; kila kitu ni tayari; njoni harusini.’
5. Lakini wao hawakujali, wakaenda zao; mmoja shambani kwake, mwingine kwenye shughuli zake,
6. na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatukana, wakawaua.
7. Yule mfalme akakasirika, akawatuma askari wake wakawaangamize wauaji hao na kuuteketeza mji wao.