Mathayo 21:8-10 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Umati mkubwa wa watu wakatandaza nguo zao barabarani, na watu wengine wakakata matawi ya miti wakayatandaza barabarani.

9. Makundi ya watu waliomtangulia na wale waliomfuata wakapaza sauti:“Sifa kwa Mwana wa Daudi!Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana!Sifa kwa Mungu juu!”

10. Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu, mji wote ukajaa ghasia. Watu wakawa wanauliza, “Huyu ni nani?”

Mathayo 21