Mathayo 19:24-27 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”

25. Wale wanafunzi waliposikia hivyo walishangaa sana, wakamwuliza, “Ni nani basi, awezaye kuokoka?”

26. Yesu akawatazama, akasema, “Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote huwezekana.”

27. Kisha Petro akasema, “Na sisi je? Tumeacha yote tukakufuata; tutapata nini basi?”

Mathayo 19