Mathayo 15:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. basi, hapaswi tena kumheshimu baba yake! Ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa kufuata mafundisho yenu wenyewe.

7. Enyi wanafiki! Isaya alitabiri sawa kabisa juu yenu:

8. ‘Mungu asema: Watu hawa huniheshimu kwa maneno tu,lakini mioyoni mwao wako mbali nami.

9. Kuniabudu kwao hakufai,maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu.’”

10. Yesu aliuita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni, mkaelewe!

11. Kitu kinachomtia mtu unajisi si kile kiingiacho kinywani, bali kile kitokacho kinywani. Hicho ndicho kimtiacho mtu unajisi.”

Mathayo 15