Mathayo 10:6-10 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.

7. Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

8. Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.

9. Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.

10. Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.

Mathayo 10