Matendo 5:18-23 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.

19. Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,

20. “Nendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya uhai huu.”

21. Mitume walitii, wakaingia hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha.Kuhani mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu na halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi, halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.

22. Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,

23. wakisema, “Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani.”

Matendo 5