Matendo 24:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Baada ya siku tano, kuhani mkuu Anania aliwasili Kaisarea pamoja na wazee kadhaa na wakili mmoja wa sheria aitwaye Tertulo. Walimwendea yule mkuu wa mkoa wakamweleza mashtaka yao juu ya Paulo.

2. Paulo aliitwa, na Tertulo akafungua mashtaka hivi:“Mheshimiwa Felisi, uongozi wako bora umeleta amani kubwa na marekebisho ya lazima yanafanywa kwa manufaa ya taifa letu.

3. Tunalipokea jambo hili kwa furaha daima na kutoa shukrani nyingi kwako kila mahali.

Matendo 24