34. Na juu ya kumfufua kutoka kwa wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi:‘Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.’
35. Naam, na katika sehemu nyingine za Zaburi asema:‘Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.’
36. Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza matakwa ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37. Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38. Kwa hiyo, jueni, ndugu zangu, kwamba kwa njia ya mtu huyu ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu;
39. na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya sheria.