16. Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
17. Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hayo maono aliyokuwa ameyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
18. wakaita kwa sauti: “Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?”
19. Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa yale maono, na hapo Roho akamwambia, “Sikiliza! Kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.