3. Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4. Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
5. Lakini Yesu hakujibu neno, hata Pilato akashangaa.
6. Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7. Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8. Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.