23. Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye alikataa kunywa.
24. Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25. Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26. Na shtaka dhidi yake lilikuwa limeandikwa, “Mfalme wa Wayahudi.”
27. Pamoja naye waliwasulubisha wanyanganyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto. [
28. Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”]