Marko 13:34-37 Biblia Habari Njema (BHN)

34. Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia na mlinzi wa mlango awe macho.

35. Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.

36. Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.

37. Ninayowaambieni nyinyi, nawaambia wote: Kesheni!”

Marko 13