35. Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36. Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37. Walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38. Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39. Basi, akaenda kila mahali huko Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40. Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba: “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41. Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka! Takasika!”