Marko 1:28-30 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika eneo la Galilaya.

29. Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.

30. Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.

Marko 1