Marko 1:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

2. Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:“Mungu alisema, ‘Namtuma mjumbe wangu akutangulie,ambaye atakutayarishia njia yako.’

3. Sauti ya mtu anaita jangwani:‘Mtayarishieni Bwana njia yake,nyosheni barabara zake.’”

4. Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.

5. Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.

Marko 1