7. Wazee wetu walitenda dhambi na hawapo tena;nasi tunateseka kwa sababu ya makosa yao.
8. Watumwa ndio wanaotutawala,wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao.
9. Chakula chetu twapata kwa kuhatarisha maisha yetu,maana wauaji wanazurura huko mashambani.
10. Ngozi zetu zawaka moto kama tanurikwa sababu ya njaa inayotuchoma.
11. Wanawake wetu wanashikwa kwa nguvu mjini Siyoni,binti zetu katika vijiji vya Yuda.