3. Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani. Akawa anahubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4. Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:“Sauti ya mtu anaita jangwani:‘Mtayarishieni Bwana njia yake;nyosheni barabara zake.
5. Kila bonde litafukiwa,kila mlima na kilima vitasawazishwa;palipopindika patanyoshwa,njia mbaya zitatengenezwa.
6. Na, watu wote watauona wokovu aletao Mungu.’”
7. Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea muikimbie ghadhabu inayokuja?
8. Onesheni kwa vitendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kujisemea: ‘Baba yetu ni Abrahamu!’ Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyafanya mawe haya yawe watoto wa Abrahamu.