Luka 24:42-45 Biblia Habari Njema (BHN)

42. Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.

43. Akakichukua, akala, wote wakimwona.

44. Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: Kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”

45. Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.

Luka 24