17. Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.]
18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (
19. Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20. Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21. lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”