Luka 23:17-21 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.]

18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (

19. Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)

20. Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;

21. lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”

Luka 23