39. Baadhi ya wale waalimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40. Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41. Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42. Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi:‘Bwana alimwambia Bwana wangu:Keti upande wangu wa kulia
43. mpaka niwaweke maadui zako kuwa kiti cha kuwekea miguu yako.’
44. Ikiwa Daudi anamwita yeye, ‘Bwana,’ basi, atakuwaje mwanawe?”