32. Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33. Watampiga mijeledi na kumuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34. Lakini wao hawakuelewa jambo hilo hata kidogo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35. Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36. Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”