Luka 12:48-51 Biblia Habari Njema (BHN)

48. Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atadaiwa vingi; aliyepewa vingi zaidi atadaiwa vingi zaidi.

49. “Nimekuja kuwasha moto duniani; laiti ungekuwa umewaka tayari!

50. Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!

51. Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.

Luka 12