48. Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atadaiwa vingi; aliyepewa vingi zaidi atadaiwa vingi zaidi.
49. “Nimekuja kuwasha moto duniani; laiti ungekuwa umewaka tayari!
50. Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51. Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.