8. Siku moja, ilipokuwa zamu yake kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9. Zakaria alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10. Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11. Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12. Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.